Читать книгу Sayari Saba - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo - Страница 5

Оглавление

Sura ya Kwanza

Bahari ya Ukimya

Jenarali Ruegra alikuwa akitazama angani kupitia shimo kubwa kwenye dirisha ndogo kwenye dambra. Ilivutia kuona mfumo mzima wa sayari wa KIC 8462852 na sayari zake saba kwenye obiti. Wakati huo, angeweza kuona tu sayari tano kati ya hizo: Sayari ya Carimea, ambayo ni nyumbani kwake, ilikuwa na anga ya kijivu, ambayo ilimaanisha ilikuwa imepangiwa nafasi ya uongozi; Medusa ilikuwa ya bluu na ya kupendeza, ambayo ilikuwa na sumaku na hatari kama wakaazi wake; Oria, ambayo ilikuwa ndogo na tasa kama mwezi, na pia ilikuwa nyeupe kutokana na akisi ya mwangaza wa Jua letu. Umbali usio mrefu kutoka Oria, kulikuwa na Sayari ya sita ambayo ilikuwa kijani kibichi, na ambayo ilikuwa na ujamii zaidi na ilikuwa imeendelea kiteknolojia miongoni mwa sayari nyingine; na Eumenide, iliyokuwa na anga ya waridi, ambayo ilikuwa ya kuvutia sawa na wakaazi wake wa kutisha.

Yote hayo hivi karibuni yatakuwa mali ya watu wa Aniki na yeye atateuliwa kiongozi mkuu. Alihitajika kuwa mvumilivu na kukamilisha mpango wake: huku akiwa na Ngozi iliyo na sheria mikononi mwake kila kitu na kila mtu atafanya kulingana na mapenzi yake.

Jenerali Ruegra alikuwa akitazama angani kupitia dirisha ndogo kwenye dambra lake na angehisi tamaa ya uongozi ikikua ndani yake. Ilikuwa mwaka wa 7692 tangu kuanzishwa kwa utawala wa Aniki. Ruegra aliamshwa ghafula kutoka kwenye ndoto ya adhama. Chombo chake cha angani kilikuwa kimegonga kitu: walikuwa wanavuka mviringo wa Bonobo. Ingekuwa bora kuelekea kwenye dambra ya kuthibiti chombo. Ingawa kutua kwenye sayari hiyo ilikuwa utaratibu wa kawaida, bado inaweza kuwa na matatizo kadhaa.

Punde tu alipoingia katika dambra ya kuthibiti chombo, alilakiwa kwa heshima na wasaidizi wake.

Utaratibu haukuwa unaenda vizuri kama ilivyopangwa awali: kuna kitu kilikuwa kimegonga meli hiyo ya angani, kama alivyohofia.

"Jenerali, eneo la 8 limeharibiwa. Jiwe limetugonga. " Nahodha akaripoti mara moja.

"Tenga eneo hilo mara moja na uendelee kuliondoa sehemu hiyo."

Nahodha aliamuru mchakato wa uokoaji katika eneo lililotengwa:

"Uokoaji wa haraka katika eneo hilo ...

Ulitenge! Usipoteze wakati wowote! " "

Afisa huyo mara moja alitekeleza amri hiyo. Hakuna aliyethubutu kumfanya Ruegra aone kuwa hatua hiyo itachukua maisha ya wanajeshi wengi bure.

Kuta nyingi zilizokuwa zikitenganisha eneo hilo kutoka kwa sehemu nyingine za meli hiyo ya angani zilifungwa. Wanajeshi wachache tu ndio walioweza kuruka kwa haraka chini ya mlango uliotenganisha eneo hilo na nyingine ili kuepuka kusombwa. Kwa bahati mbaya, walishuhudia wenzao, ambao walikuwa wameishi pamoja hadi dakika chache zilizopita, wakipoteza matumaini walipogonga kuta hizo na kisha wakatoweka.

Utengaji wa eneo lililoharibika ulikamilishwa, na eneo hilo likaachwa.

Vyombo vyote vya angani vya Carimea vilikuwa vya angani na vilikuwa na umbo la mdudu mkubwa wa trilobiti. Vilikuwa vimegawanya kwa vipande vipande ili eneo fulani liondolewe kwa haraka linapoharibika. Kwa njia hii, wafanyikazi wataafikia matokeo mazuri wakati wa vita. Sehemu zote mbili za katikati na mkia, ambazo zilikuwa na umbo la ganda la chaza, zinaweza kuondolewa. Dambra ya kuthibiti chombo hicho, inayoshirikisha sahani kubwa na sura ya nusu mviringo ambayo inakuwa na pembe nyingi katika sehemu nyingine na kuwa ‘mgongo’ wa chombo hicho, haiwezi kuondolewa.

Zilikuwa zimezungukwa na mnyoosho usio na mwisho zilizoundwa na miviringo kubwa ya kijivu ambayo ilikuwa imezunguka sayari ya Bonobo. Miviringo hiyo ilikuwa inajumuisha vifusi vikubwa vilivyosababishwa na kifo cha kimondo ambacho kilikuwa kimesonga karibu na KIC 8462852.

Bonobo, ambayo ni sayari ya pili iliyo mbali kutoka kibete, pia ilijumuisha donge ambalo lilikuwa limekusanya vifusi vingi. Kwa njia hii, ilikuwa imeacha sayari ndogo ya Enas na ilikuwa imeunda mandhari ya kiajabu katika galaksi yote.

Sayari hiyo ilipatikana katikati ya miviringo hiyo. Ilikuwa ina mali nyingi sana na tofauti hivi kwamba ilitumika kama hifadhi ya kifalme ya Aniki ya uwindaji, watumwa na vifaa. Watu wake ambao walikuwa kama binadamu walikuwa wamekwama katika mwanzo wa utawala wao. Watu wa Bonobo walitembea wima, walikuwa na miguu ya yenye viungo vya kushika na miili yao ilikuwa na manyoya.

Walikuwa kubwa kama masokwe lakini hawakuwa werevu na walikaa kama watoto. Wangezaa haraka na walikuwa na nguvu, ambayo ingawafanya wakimilifu.

Bonobo ilikuwa sayari ya pekee ambayo ilitwaliwa na wana-Aniki ambayo ilisalia chini ya utawala wao. Na ni kwa sababu tu sayari hizo mbili zilikuwa zinafanana na zilikuwa zinazunguka KIC 8462852.

Carimea ilikuwa imeweza kutwaa utawala wa sayari nyingine pia, lakini kila mara walikuwa wanapoteza uthibiti kutokana na uasi uliochochewa na muungano wa sayari hizo nne, ambazo lengo lao lilirahisishwa na kuwa karibu kwa mzingo.

Meli ya angani kilitua kwa wakati ufaao. Katika makao makuu, vifaa tayari vilikuwa vimetayarishwa kwa mgao. Ruegra alishuka chini ili kuongea tu na Mastigo, Gavana wa eneo hilo. Jenerali huyo hakumpenda huyo mtu wa Evic hasa, lakini uongozi wake kwa wakaazi ulikuwa na ufanisi. Alikuwa wa kabila maarufu huko Carimea.

Wa-Eviki walikuwa wakubwa, reptilia wa kijani-kijivu ambao wangetembea kwa miguu yake ya nyuma iliyokuwa minene na yenye nguvu. Walikuwa wadogo kidogo kuliko wa-aniki isipokuwa nyuso zao, ambazo zilifunikwa kabisa na magamba. Nyuzo zao ambazo nusu zilikuwa na umbo la duaradufu zingenyooka nje kutoka maskio na kuchukua umbo la nusu kengele. Hawakuwa na mashavu yoyote na mapua yao yaliyokuwa kama nyoka na hayakuonekana kabisa. Walikuwa wakali, lakini hawakuwa werevu hasa, walikuwa kabila pekee ambalo lingengangania mamlaka na Wa-aniki kwa idadi na nguvu. Walivaa koti refu la kiuno la hariri ambalo linafunikwa na miguu yao na ambayo inafungwa kwa vifungo kwenye kifua. Ili kupata usaidizi wao, Ruegra alikuwa amemteua mmoja wao kuwa Gavana wa Bonobo.

Jenarali alikaribishwa kwa utukufu kwenye ukumbi wa glasi kwenye jengo la serikali, ambako kuna mazingira mazuri ya kitropiki ya kupendeza. Ulikuwa usiku wa kustaajabisha na anga ilikuwa imewashwa kwa akisi wa miviringo hiyo.

Ruegra alikuwa akitazama kupitia glasi iliyokuwa ikiakisi picha yake.

Rangi ya mwili wake thabiti, iliyokuwa imefunikwa na ngozi kavu, ambazo zingebadilisha rangi kulingana na mazingira. Sura haikuweza kutambulika kati ya miti iliyo nje. Taji ngumu iliyotengenezwa kwa tishu za karatini na ilikuwa na urefu wa Kudus 30 au inchi 11 ilikuwa imepamba sura yake, kuanzia kichwa. Taji hiyo ingefunguka kama kuna hatari na inakuwa silaha ambayo Wa-Aniki walitumia wakati wa mwanzo wa utawala wake kumtisha adui. Inapofunguliwa kwenye mkono, ingetumika kama ngao.

Kutokana na uso wake wa mviringo ngozi kavu zingesinyaa na kuwa sawa kwa rangi. Chini ya paja la uso wake, nyusi na kobe zake za bluu za karatini hufanya macho yake kubwa ya kijani kibichi na mashavu yake laini yenye rangi yaliyodhihirika. Pua lake kubwa lililolemaa, kama la bondia, lilihitiliafiana na sura yake. Mdomo wake uliwiana vizuri: mdomo wake wa kijani ulikuwa kubwa na nono.

Waaniki walikuwa wakubwa zaidi kwa urefu miongoni mwa watu wote katika mfumo wa jua na sayari zake na kwa sababu hiyo daima wamekuwa juu katika piramidi ya Wanyama wawindaji.

Sawa na Wa-aniki, Ruegra kwa kawaida huvaa sketi iliyona vipande viwili vilivyopasuliwa ambavyo vingeonesha Ngozi kavu kwenye mwilini wake. Begani angevaa rasi, ambayo inadhamiriwa kuonesha tabaka na majukumu yake. Rasi yake ilikuwa na rangi ya dhahabu, ilioashiria cheo chake cha amri na ilipambwa na sura ya rangi ya moshi-kijivu na nakshi ya rangi sawa ilioonesha ndege ya uwindaji wa Atrex.

"Ninasalimu asiyeweza kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Unakaribishwa kila wakati katika nchi yetu, jenarali wangu. Safari ilikuwaje?" akamsalimu Mastigo kwa kumwinamia kidogo.

"Ilikuwa nzuri. Ujumbe unaendelea kwa njia nzuri." Ruegra akadanganya. "Nahitaji tu kupumzika. Pete hizo za sayari hufanya meli ya angani kutetemeka kidogo." Alisema ili aachane na mzungumzaji.

Mastigo alimpa kinywaji cha matunda ya huko ili aburudike baada ya safari ndefu baina ya sayari. Ilikuwa afadhali kwa Jenerali kuketi kwani alihitajika kuripoti tukio lisilo la kawaida.

"Ninatukio lisilo la kawaida ambalo linahitaji kuwasilishwa kwako. "Siku mbili zilizopita za Bonobo, tuliona chombo cha angani cha biashara kilipokuwa kikiingia eneo letu bila ruhusa. Walinzi hawakuweza kuisimamisha kwa wakati ufaao. Kwa hivyo, ilitumbukia katika Bahari ya Unyamavu kabla hatujatathmini hatari zake halisi.

Tumefanya utafiti na tumepata kwamba mmiliki amekiuza kwa mwanamke mmoja wa Eumenide. Nimetuma askari kadhaa wa doria kuchunguza eneo linalodaiwa kutua. Lakini kama unavyojua, haiwezekani kupokea mawasiliano ya aina yoyote kutoka Bahari ya Unyamavu. Kwa hiyo, tunachotakiwa kufanya ni kusubiri."

Ruegra alikasirishwa na jinsi Gavana alivyoshikilia ukweli huo usio na maana na akauliza:

"Ni nini cha ajabu kuhusu hayo? Sielewi..."

"Angalia mahali ilikuwa inaelekea..." akasema Mastigo akionesha ramani ya Bahari ya Unyamavu.

"Hapa ndiko mahali ngome takatifu ya Bonobo inapopatikana..." Ruegra akanong’oneza.

"Ndio sababu nilichukua huru wa kuripoti tukio dogo kama hilo. Nimetuma timu kuchunguza eneo hilo. Inaweza kuwa ililingana tu, lakini ni heri kuwa salama kuliko kusema pole. Mahali hapo pamejaa miujiza. Ingekuwa makao makuu mazuri kuanzia migogoro, ukizingatia ukosefu wa mawasiliano na ishara za rada. Ni kama shimo jeusi.

"Unaweza kuwa sahihi. Endelea kunisasisha, Mastigo. Sasa ni bora ikiwa nitapumzika. Kesho tutaondoka alfajiri."

Usiku huo Ruegra alikuwa na vitu vingine vya kufikiria. Baada ya kurudi chumbani kwake, aliketi kwenye sofa laini na kujipatia kinywaji aina ya Sidibé, pombe kali ya kienyeji inayopatikana kwa cacti. Alikuwa akitazama angani huku fikra zake zikikimbizana kama mawimbi kabla ya dhoruba.

Safari ambayo alikuwa tu amemaliza imekuwa ya janga kabisa, kinyume na kile alichokuwa amemwambia mshirika wake anayemwamini.

Alikuwa amezuru Mwezi wa sayari ya Enas, haswa kwa koloni ya uchimbaji madini ya Stoneblack, kambi ndogo inayofahamika sana kwa marumaru yake. Jenarali huyo alikuwa akihitajika kukutana na mtu ambaye babaye mwenyewe alikuwa anamheshimu sana: adui wa zamani wa Carimea.

Koloni hiyo ilitawaliwa na kabila la Triki. Walikuwa watu kutoka Carimea, kama Wa-aniki, lakini walikuwa na ushawishi wa pili kwenye usimamizi wa sayari hiyo.

Walikuwa wamejitolea kuhudumu, lakini hawaaminiki. Walikuwa wamejidhihirisha kuwa wasaliti mara tu upepo unapobadilisha mwelekeo. Hata rafiki zake mwenyewe wangeweza kupanga njama dhidi yake kwenye Mwezi huo. Kwa hivyo, ilibidi kufanya ukaguzi huo uonekane kama ziara ya ghafula akiwa na nia ya kurudisha baadhi ya visukuu vya mwezi kwa nduguye wakati wa kurudi.

Ruegra alitembea mbele ya maafisa hao. Alileta kiwiko chake karibu na bega lake na huku mkono wake ukiwa sambamba na sakafu na karibu na kinywa chake, akawasalimia. Ishara hiyo ilionesha ukimya mbele ya amri yake pamoja na utii kamili. Walikuwa bado wamenyamaza mbele yake.

Koloni hiyo ya uchimbaji madini iliajiriwa kama wahalifu wanaofanya kazi ya lazima na wafungwa wa kivita kufanya kazi kwa gharama rahisi. Walinzi hao wangemlinda mtumwa mmoja hasa...Alikuwa mtu wa Ruegra. Sio tu kwamba alikuwa mtumwa wa kiwango cha juu, lakini pia alikuwa amepata heshima kutoka kwa watumwa wenzake na aliweza kuwaakilisha.

Jenarali huyo, aliyeandamana na nahodha na kufuatiwa na wanajeshi, aliwekwa kwenye chumba cha kupumzika na cha kutolea amri, amchacho kilikuwa kimetengewa afisa huyo.

Nahodha huyo alitoa heshima zake na kuuliza iwapo angetaka kitu.

Ruegra hakupoteza wakati wowote. Alikataa ofa hiyo na akaamuru:

"Ninataka kuthibitisha hali ya wafungwa wa kisiasa ambao walichukuliwa wakati wa vita dhidi ya Sayari ya Sita. Wacha niongee na afisa mwenye cheo cha juu."

"Jenarali Wof?"

"Ndio, haswa. Mlete kwangu. " "

"Ndio, bwana."

Kamanda akaguna kwa walinzi na dakika chache baadaye walirudi chumbani akiandamana na mtu wa makamo. Alionekana mchovu na kukosa nguvu, lakini bado alikuwa na kiburi na sura ya mpiganaji asiye na hofu.

"Tuacheni." akamrishwa Ruegra.

Alisalia pekee akiwa na adui mwenye akili kali. Alikumbuka kuwa wakati wa vita alikuwa ameweza kubadilisha hali mbaya ambayo ilikuwa imetabiri kifo chake, shukran kwa kufikiria kimkakati na licha ya kuwa na watu wachache kutoka Sayari ya sita chini ya utawala wake.

Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kuzungumza. Alikuwa tayari amewaza kuhusu mikakati kadhaa wakati wa safari yake. Alijua kwamba haingewezekana kumshika adui yake bila kufahamu. Ilikuwa wakati wa kuchukua mmoja na kuanza makabiliano.

Aliamua kuendelea na ibada hiyo ya kumsifu akitarajia kwamba uzee wake na uchovu wake umemfanya kudhoofika zaidi.

"Nakusalimu, Wof. Ninaweza kusema kwamba hauonekani vibaya licha ya kutopewa matibabu bora. Hata hivyo nimeamrisha upatiwe vitabu na elimu. " "

"Muda mrefu sijakuona." alisema Wof, akimtazama jenarali huyo na macho yake ya kina na meusi. "Ni nini kilikuleta mahali hapa ambako imesahaulika na mwangaza, ambako giza inatawala?"

"Nilikuja hapa kuongea nawe kuhusu baba yangu. Nakumbuka kuwa nikiwa mtoto angefikria kuhusu Ngozi ambayo ulijua siri zote kuihusu. Sasa kwa kuwa ninazeeka, wakati mwingine ninafikiria kumhusu na kushangaa iwapo kuna ukweli kuhusu hadithi hiyo."

Wof alijaribu kuficha ushangao wake kwa kupapasa nywele zake hizo ambazo zilikuwa zinampa sura uso wake nyeusi.

"Baba yako alikuwa akisema ukweli, lakini inavyoonekana, hakufikiria kwamba ulikuwa mwaminifu wa kutosha kujua maelezo yote.

Pia alijua siri zote ambazo hazijazungumziwa. Ruegra alishangaa. Baba yake alikuwa ametaja siri hiyo mara nyingi, lakini hakuwahi kuwa na hamu ya kufichua.

"Nini mbaya, Jenerali? Unashangaa kwanini hakukuambia zaidi kuihusu?"

"Labda umri wangu mdogo na msukumo wangu ulinifanya msikilizaji mbaya."

"Afadhali niseme kwamba tabia yako ni hamu ya kuwa na mamlaka na utawala wa kijeshi."

"Mamlaka ni muhimu kudumisha utulivu na uimara." Akasisitiza Jenarali huyo, baada ya kusimama akiwa amekasirika.

"Una imani na utaratibu, ukiwa umeajiriwa kuhudumia mtu mmoja na kwa utulivu wa kabila moja." akajibu Wof.

Ruegra alianza kutembea kwa uwoga. Alikuwa tayari amepoteza uvumilivu wake, lakini alijua vizuri kuwa hakuna mateso au ulafi ambao ungefanya kazi kwa mtu ambaye alikuwa ameketi mbele yake. Tumaini lake la pekee lilikuwa kupata uaminifu wa mtu huyo.

Alianza kuwa mjanja na kudanganya:

"Unajua, kwa kweli ninamheshimu baba yangu. Wakati nilipokuwa mdogo ulikuwa ukisema kwamba ninafanana naye... Wakati huo, nilikuona kama bwana...."

"Nini inakufanya kufikiria kwamba nitafichua jinsi ya kupata ngozi hiyo? Usafi huo uliokuwa nao utotoni ulipotea haraka, Ruegra, na nia ya kujithibitisha ilichukuliwa na kiu ya mamlaka."

"Mimi si Aniki ambaye unamkumbuka wakati wa vita. Nitajua kuthibiti mamlaka kwa usawa. Baba yangu alifanya makosa kwa kukosa kuniambia kila kitu." "Jenerali alisema kwa hasira nyingi.

"Ikiwa ilibidi uje kwangu, inamaanisha kuwa haukustahili kuaminiwa na baba yako. Ni baba wa aina gani anayeficha maarifa kutoka kwa mwanawe? Kuna taabu katika ishara zake. Nani aliyebora kuliko yeye alikujua na mimi ni nani kufichua kila kitu kwako na kupuuza kabisa tathmini yake? Kama unavyoona siwezi fanya chochote lakini kuheshimu nia yake na kuheshimu kumbukumbu yake." Alisema Wof. Kisha alisimama na kusema kwaheri kwa mnyongaji wake.

Tukio hilo halingeondoka katika akili ya Jenarali, ambaye aliendelea kutazama angani akiwa na glasi mkononi kwenye usiku huo wa Bonobo uliokuwa joto.

Asubuhi iliyofuata, Ruegra alichunguza binafsi kazi ambayo ilikuwa imekamilishwa kubadilisha sehemu iliyoharibika ya chombo cha angani.

Mastigo alikuwa amefuatilia vizuri na mafundi wake walikuwa wamefanya kazi nzuri kama kawaida. Wakaondoka kwa wakati uliowekwa na kurejea nyumbani.

Siku zilikuwa zikipita na Ruegra alikuwa na haraka ya kurudi nyumbani. Aliogopa njama, ingawa kakaye, ambaye alikuwa akiongoza wakati hakuwepo, atampa Jenarali ripoti za kila mara kuhusu hali hiyo. Hapakuwa na kitu cha kuwa na wasi wasi nacho. Carimea ilikuwa mchanganyiko wa jamii. Makabila tofauti walikuwa wakipigania utawala dhidi ya Wa-aniki, lakini Wa-aniki walikuwa wamewaondoa idadi inayodhihirika ya wapinzani wakati wa utawala wao. Ilikuwa imeanzishwa na vikundi kadhaa vya mfumo tofauti wa jua, wengi wao walikuwa watalii, watafutaji wa bahati au wafungwa wa awali ambao walikuwa wakitafuta ardhi kuanzisha maisha yao upya. Sehemu ndogo tu kati yao walitoka kwenye sayari hiyo. Kwa kweli, watu wa sehemu hiyo walikuwa wametawaliwa kishenzi na kutengwa.

Njiani wakirudi, huku akiwa ameketi katika kiti cha kuthibiti chombo kwenye dashibodi, Ruegra alikuwa akifikiria kuhusu maneno ya Wof. Kwamba "Baba yangu alijua" iliendelea kusikika akilini mwake.

Kisha kwa ghafula, akafikiria nyakati zote baba yake angeondoka wakati wa msimu wa uwindaji na kabla ya vita vyote. Mahali alipenda kwenda ilikuwa kwa kweli ardhi ya Bonobo, haswa kwa Bahari ya Unyamavu.

Wakati fikra hizo zilikuwa zikitembea kwenye akili yake, alipata utambuzi wa kuangaza na kufikira:" Mbona sijafikiria kuhusu haya awali?" Kitu au mtu huku huenda alimpa taarifa zaidi kuhusu ngozi hiyo iliyo na siri.

Alihusisha uhisi wake na ripoti ya Mastigo kuhusu chombo cha angani cha kibiashara. Labda mtu alikuwa mbele yake.

Aliamuru kubadilisha njia mara moja. Walikuwa wanarejea huko Bonobo.

Mastigo, aliyekuwa ameshangaa baada ya kuwaona wakirudi, alikimbia kuelekea chombo hicho cha angani.

"Ninasalimu mtu ambaye hawezi kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Jenerali, mbona umerudi?"

"Nimetafakari kuhusu kutua kwa chombo hicho cha angani, na imenishawishi kurudi na kushughulikia binafsi hali hiyo."

"Kwa mara nyingine, umefanya jambo la busara. Wataarifu wangu hawakurejea Bonobo. Kwa hivyo, niliamua kuzuru eneo hili mimi binafsi. Niligundua kuwa walikuwa wameondolewa na watu wasiojulikana."

Ruegra alikuwa akitumaini kuwa Gavana wake hajaharibu uwezekano wote wa kupata taarifa kwa kuwa alijua njia zake.

"Hakuna kilichoachwa huko." akaripoti Mastigo mara moja, ambaye alikuwa akionekana kuridhika kama mtoto ambaye alitesa mawindo yake madogo.

Ruegra alijizuia kumshambulia msemaji wake na kumwuliza mahali wafanyakazi wake walikuwa wameenda.

Mastigo alichukua pumzi mzito, akifahamu kuwa haitakuwa Habari njema.

"Hatukuweza kuipata. Lazima wamekimbia."

"Sio tu uliharibu ushahidi wote, lakini pia uliwaacha wafanyakazi kutoroka! Ulikuwa huna ujuzi wewe! Nipeleke huko!"

Kisha, baada ya kufikiria tena alitambua kuwa haitakuwa wazo nzuri kumruhusu Mastigo kufahamu kuhusu mipango yake.

"Niandalie wafanyakazi. Nitaondoka kesho bila wewe."

Sayari Saba

Подняться наверх